Powered by Blogger.

serengeti club of shotokan karate


Sensei yahya Omar Mgeni ni miongoni mwa waalimu wachache hapa nchini Tanzania wenye sifa kima zake, ni mwalimu mwenye kujitolea katika kueneza mchezo wa karate na misingi yake yaDOJO-KUN na NIJU-KUN ni mwalimu pekee anayefundisha karate kama BUDO, ni mwenye kushirikiana na waalimu mbalimbali. 

Anashaurika, mzalendo na amekuwa ni chachu ya kuzaliwa kwa chama cha karate Shotokan "TASHOKA" (Tanzania ShotokanKarate) pia kuzaliwa kwa T.K.F (Tanzania Karate Federation).

Ameanza safari ya kujifunza Shotokan Karate mnamo mwaka 1986 chini ya kocha Sensei Mustafa Ahmed nchini Kenya, mpaka mwaka 1989 akiwa na 1st kyu Brown Belt, kisha alipata
Scholarship kwenda Egypt ambako alijiunga na klabu ya polisi “NAD-EL-SHURTA” iliyoko Abbasiya Cairo, hapo aliendelea kujifunza chini ya kocha wa timu ya taifa ya Egypt wakati ule sensei kapteni Zakaria, Mnamo mwaka 1993 alifanya grading ya Sho-dan iliyosimamiwa na E.K.F (Egypt Karate Federation).

Mnamo mwaka 1994 alishiriki semina ya urefa iliyosimamiwa na E.K.F iliyofanyika Alexandria na mwaka 1995 alishiriki semina ya urefa iliyosimamiwa na E.K.F iliyofanyika Port Said.

Ameshiriki tournament nyingi za vilabu na vyuo nchini Egypt na kuchukua medali na vikombe. Mwaka 1996 alirejea nchini na kuasisi klabu ya Karate “Iringa Karate Shotokan Club” kutokana na kutokuwepo na vilabu vinavyozielewa sharia za W.K.F wakati ule alilazimika kwenda Kenya kuomba ushiriki wa mashindano mbalimbali huko.

Mnamo mwaka 1999 alipeleka timu ya mkoa wa Iringa kushiriki mashindano ya vilabu- interclub (Coast championship) timu ya Iringa ilifika robo fainali baada ya kutolewa na timu ya (Navy). Mnamo mwaka 2000 alipeleka timu Mombasa Kenya ya watoto under 15 na kurudi na medali ya dhahabu. Mnamo mwaka huu Sensei Yahya O Mgeni alifanya grading Ni-dan iliyosimamiwa na Coast Karate Association.

Mwaka 2002 Iringa ilipokea timu toka Kenya na kucheza nayo Friendly match na mwaka 2003 Iringa ilipokea timu tena toka Kenya na kucheza nayo. Mwaka 2005 Sensei Yahya O Mgeni alihama Iringa na kuhamia Dar es salaam na kuasisi “Serengeti Shotokan Karate Club” Mwaka 2006, mnamo mwaka 2007 Iringa ilishiriki “Sababa Tournament” iliyoandaliwa na ubalozi wa Japan chini ya usimamizi wa mkufunzi kutoka Japan Sensei Yushi Fuji na kutoa ushindi, Mnamo mwaka 2008 Serengeti ilipata mwaliko wa shindano la karate “Japan Karate Championship” team na individual lililofanyika Don-bosco chini ya usimamizi wa Shihan Mishaly toka South Africa, Serengeti ilikuwa mshindi wa kwanza timu na individual (mshindi wa kwanza na wa pili).

Mnamo mwaka 2009 ubalozi wa Japan uliandaa shindano lililosimamiwa na Sensei Kaneto, Serengeti Shotokan ilichukua nafasi ya kwanza kumite na kata.
Mnamo mwaka 2012 Sensei Yahya O. Mgeni alipeleka timu ya Tanzania kushiriki mashindano ya dunia “World Karate Tournament” yaliyofanyika Malindi Kenya na kushirikisha Zaidi ya nchi kum. Mwaka huu Serengeti ilihudhuria Semina ya kimataifa ya Karate iliyosimamiwa na Shihan Farid Al-shuhaiby Chief instructor ISKF Oman iliyofanyika Zanzibar.

Mnamo mwaka 2013 kwa juhudi zake Sensei Yahya alifanikiwa kupata uanachama wa shirikisho la Karate I.S.K.F- International Shotokan Karate Federation lenye makao yake makuu marekani chini ya Shihan TERIYUKI OKAZAKI SENSEI 10TH DAN na mnamo mwaka huo Sensei Yahya O. Mgeni alifanya grading ya kimataifa ya San- dan chini ya Shihan Farid Al-shuhaiby 7th Dan na walifanya wanafunzi wake Sho-dan , Ni-dan, na San-dan.

Hadi sasa Sensei Yahya O. Mgeni ndiye sensei mwenye wanafunzi wengi Tanzania, anao black belt 50 na kyu ranks 200 na ni sensei wa kwanza mwenye vilabu vingi Tanzania.


Share
Tweet
Pin
Share
4 comments

 VILABU VYA ISKF TZ NA WAALIMU WAKE

Vilabu wanachama wa ISKF ni:
  • IRINGA SHOTOKAN KARATE
Chini ya wakufunzi:     
- Sensei Swalehe Bakari 2nd Dan
- Sensei Mohamed          2nd Dan
- Sensei Kasim Mdota     2nd Dan

  • SINGIDA SHOTOKAN KARATE
Chini ya wakufunzi:  
- Sensei Salumu Mussa           2nd Dan  
- Sensei Makuka A. Makuka    2nd Dan

  • MBEYA SHOTOKAN KARATE
Chini ya mkufunzi      
- Sensei Mawazo Sondes          1st Dan

  • DODOMA SHOTOKAN KARATE
Chini ya wakufunzi    
- Sensei Venance Vahaye   
- Sensei Elias Tete

  • MOROGORO SHOTOKAN KARATE
Chini ya mkufunzi      
- Tito Kitundu                       2nd Dan

  • KIRINJIKO SHOTOKAN KARATE
Chini ya mkufunzi     
- Sensei Ayub S. Mghewa   2nd Dan

  • GONGOLAMBOTO SHOTOKAN KARATE (D.S.M)
Chini ya wakufunzi   
- Sempai Swed Ramadhan  
- Sempai Swalehe Kiswabi
- Sempai Badru Mvumbagu

  • SERENGETI SHOTOKAN KARATE (ilala C.C.M D.SM)
 Chini ya wakufunzi   
- Sensei Yahya Mgeni 
- Sensei Munir Swaleh
Share
Tweet
Pin
Share
No comments

About me

Created with by ThemeXpose | Distributed By Gooyaabi Templates